Posts

Showing posts from April, 2017

GBROS DE VOICE AACHIA NGOMA MPYA IITWAYO "KALE"

Image
Ngoma mpya iendayo kwa jina la "KALE" imekuwa ni nyimbo ya kipekee yenye beat nzuri na mashairi yaliyopangiliwa iliyoimbwa na msanii Gbros De Voice na kutengenezwa chini ya producer Fraga ndani ya Uprising Music Studios . Bongoka BlogSpot ikiwa na team yake ilimtafuta msanii huyo chipukizi baada ya kusikia nyimbo yake yenye ujumbe mzuri na kutaka kujua ni nini kisa cha yeye kutunga nyimbo hiyo. Kutokana na maelezo yaliyopatikana kutoka kwa msanii huyo anaevuma kwa sasa jijini amesema kuwa ameandaa nyimbo hiyo maalum kwa ajili ya kuwakumbusha MABINTI  wote wenye tabia nzuri kuwa TABIA zao ndio chachu katika  MAHUSIANO yao kudumu. Pia msanii Gbros De Voice amesema hivi karibuni ataupload nyimbo hiyo nzuri kwa ajili ya mashabiki na watanzania wote kuipakua( download ) hapa hapa bongoka.com . Zaidi sana ameomba support na kuupokea mziki wake anaoufanya kwani unaelimisha na kuburudisha jamii ya lika zote. Published By www...

Habari kamili kupatikana kwa Roma

Image
    Msanii wa muziki wa kizazi kipya Roma Mkatoliki                        Dar es Salaam. Msanii Ibrahim Musa maarufu kama Roma Mkatoliki amepatikana na sasa yupo katika kituo cha Polisi cha Oyesterbay jijini hapa. Kaka wa Roma,Omar Musa amesema Roma alirudishwa nyumbani saa tisa alfajiri leo, na kwa sasa yupo kituo cha Oyesterbay.  Hata hivyo Omar hakutaka kueleza kwa kina kuhusu kurejea kwa Roma akisema kuwa hadi familia itakapotoa tamko. Roma na wenzake wanne, walitekwa wakiwa katika studio za Tongwe, zilizopo Masaki, jijini hapa hivi karibuni. Source by Mwananchi.co.tz