Mchezaji soka wa Cameroon afariki uwanjani

  • 7 Mei 2016

R.I.P Mr Patrick Ekeng
Mchezaji wa soka ya kimataifa kutoka Cameroon, Patrick Ekeng, amefariki baada ya kuanguka uwanjani katika ligi ya Romania.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alipoteza fahamu dakika saba tu baada ya kuingia uwanjani kuchukua nafasi ya mchezaji mwingine katika timu yake ya Dinamo Bucharest katika mji mkuu wa taifa hilo, Bucharest.
Hakuwa amegusana wala kukaribiana na mchezaji mwingine alipoanguka uwanjani.
Matabibu walimkimbiza hospitalini ambako madaktari walijaribu kumfufua kwa zaidi ya saa moja bila kufaulu.
Kwa muda wa miaka michache iliyopita wachazaji kadhaa Waafrika wamefariki walipokuwa wakicheza uwanjani.

Comments

Popular posts from this blog

Habari kamili kupatikana kwa Roma